Fabiani 255

Fabiani 255

Jisomee Makala za Afya na Mapenzi Kila Siku

Friday, May 13, 2022

YAFAHAMU MAMBO YANAYOWEZA KUSABABISHA KIFO WAKATI WA TENDO

May 13, 2022
YAFAHAMU MAMBO YANAYOWEZA KUSABABISHA KIFO WAKATI WA TENDO
MATUKIO ya watu kupoteza maisha ghafla wakati wa tendo, yamekuwa yakiripotiwa mara kwa mara lakini ni wachache wanaoweza kuwa wanajua ni nini husababisha tatizo hili huku wahanga wakubwa wakiwa ni wanaume.

Kiasili, tendo la ndoa limeumbwa kwa ajili ya kuwafurahisha wanandoa na kuzaliana, yanapotokea matukio ya watu kufa wakati wa tendo, watu wengi huanza kuogopa na wengine kuishia kupata misukosuko kutoka kwenye vyombo vya dola, vifo hivyo vikihusishwa na ukatili wa kijinsia, jambo ambalo mara nyingi huwa si sahihi.

Wataalamu wa masuala ya afya, wamefanya utafiti na kuja na sababu mbalimbali zinazoweza kusababisha mtu akapoteza maisha ghafla wakati wa tendo la ndoa kama ifuatavyo:

1. MATUMIZI MABAYA YA DAWA
Wanaume mara nyingi hutumia dawa za kitamaduni, za mitishamba ili kuwasaidia kuwa thabiti wakati wa tendo hilo. Wengine huzichanganya na pombe wakiamini kuwa zitawasaidia katika kuongeza nguvu za kiume na hivyo kuwa na uwezo wa kujamiiana kwa ufanisi zaidi.

Wakati mwingine, baadhi ya wanaume huvuta sigara, hutumia dawa za hospitali bila maelekezo ya daktari na kutumia mihadarati ili kuongeza nguvu zao za kiume.

Wasichokijua wengi ni kwamba dawa zinazoaminika kuongeza nguvu za kiume, nyingi huwa na kemikali iitwayo ‘Nitrate’ (Naitreti), ambayo inaweza kusababisha shinikizo la damu na kusababisha kifo cha ghafla wakati wa tendo hilo.

2. MARADHI YA MOYO
Matatizo ya kiafya sio jambo linalopaswa kupuuzwa inapokuja katika suala la kushiriki mapenzi. Mtu mwenye historia ya ugonjwa wa moyo anaweza kufa wakati wa tendo hilo kwa sababu moyo wake utafanya kazi ngumu kuliko kawaida wakati wa kawaida.

Sababu za mara kwa mara za magonjwa ya moyo, hususani kwa wanawake wenye zaidi ya miaka 50 na wanaume wenye miaka arobaini ni shinikizo la damu, uvutaji wa sigara, kisukari, kiharusi na magonjwa mengine. Sababu nyingine ambayo mara nyingi husababisha magonjwa ya moyo ni msongo mkubwa wa mawazo.

Mshtuko wa moyo wakati wa tendo la ndoa mara nyingi huwakumba wanaume kuliko wanawake kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zilizofanyika. Hata hivyo, idadi ya watu wenye matatizo ya moyo ambao hupoteza maisha wakati wa tendo, huwa ni ndogo.

Utafiti unaonesha kwamba ni visa 34 tu vya mshtuko wa moyo kati ya 4,557 hutokea wakati au ndani ya saa moja ya kujamiiana na 32 ya wale walioathiriwa walikuwa wanaume.

Sumeet Chugh mtaalamu wa afya kutoka Taasisi ya Moyo ya Cedars-Sinai Heart Institute alisema utafiti wake ni wa kwanza kutathmini shughuli za kujamiiana kama sababu inayoweza kusababisha mshutuko wa moyo na utafiti wake ulichapishwa katika ripoti ya BBC Novemba mwaka wa 2017.

Utafiti wake huo uliwasilishwa katika mkutano wa American Heart Association wakati wa kutathmini vichocheo vinavyosababisha mshtuko wa moyo.

Sehemu ya maelezo yake inasema mtu huweza kupoteza maisha wakati wa tendo endapo moyo utapata matatizo na kuacha kupiga, jambo ambalo husababisha mtu kupoteza fahamu na kushindwa kupumua na iwapo hatapewa huduma ya kwanza kwa haraka, uwezekano mkubwa ni kwamba atapoteza maisha.

3. MATUMIZI YA KUPINDUKIA YA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME
Sababu nyingine inatajwa kuwa ni matumizi ya kupindukia ya dawa za kuongeza nguvu za kiume kama Viagra. Dawa hizi zimekuwa zikiuzwa katika maduka mbalimbali ya dawa duniani, kwa lengo la kuwasaidia wanaume hususan wenye magonjwa yaliyoathiri nguvu zao za kiume kuweza kurejesha uwezo huo.

Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, dawa hii inapaswa kutolewa na daktari kwa vipimo vinavyohitajika kulingana na tatizo lenyewe la kiafya.

Hata hivyo, kutokana na upatikanaji kwa njia rahisi wa dawa hizi, baadhi ya vijana na wanaume wamekuwa wakizinunua kiholela kwenye maduka ya dawa na kuzitumia ili kuwaridhisha wapenzi wao.

Kwa mujibu wa wataalam wa afya, matumizi yasiyofaa ya dawa hizi yanaweza kusababisha matatizo ya moyo na hivyo kuchochea kutokea kwa kifo wakati wa tendo hilo.

LIKE UKURASA HUU UKITUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK USIPITWE MAKALA NA MENGINE MENGI

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO

KWA TELEGRAM👇BONYEZA HAPA
Read More

Thursday, May 12, 2022

MADHARA YA KUFANYA MAPENZI SANA

May 12, 2022
MADHARA YA KUFANYA MAPENZI SANA
WATAFITI wa masuala ya afya na saikolojia wanasema tendo la ndoa ndilo tendo ambalo humpa furaha kubwa zaidi binadamu na endapo atafanya tendo hilo kwa amani, utulivu na furaha huku wakieleza kuwa kufanya mapenzi kuna faida nyingi.

Lakini linapokuja suala la kuzidi kiasi unapata matatizo ya msingi ambayo huleta madhara tena kwa watu wanaoendekeza sana ngono katika maisha yao ya kila siku.

Kuna mtu hawezi kabisa kulala bila kufanya mapenzi, hawezi kupitisha siku bila kufanya ngono, wengine wanashindwa kuvumilia angalau siku mbili au tatu. Mtu ana mke, anataka kila siku afanye naye tendo la ndoa eti kwa sababu tu ni haki yake na hakuna wa kumzuia kufanya hivyo, sababu ametoa mahari.

Jambo hili linaweza kuwa jema kwa upande mmoja, lakini tafiti zinaonyesha kwamba miongoni mwa kesi za watu wanaolalamika kupoteza hisia za kimapenzi hutoka, wengi wao wapo katika kundi la watu wapenda ngono kupita kiasi (wanaume na wanawake).

Wanawatolea mfano makahaba ambao wanafanya mara kwa mara, watu kama hawa wanatajwa kuwa hawana hisia za kimapenzi, hata kama zipo ni kiwango kidogo sana, wanafanya kwa sababu ni biashara jambo ambalo ni hatari kwa afya na saikolojia yake.

Licha ya tatizo hilo, yapo madhara mengine mengi ambayo mtu asiyekuwa na kiasi katika tendo la ndoa anaweza kukabiliana nayo, hivyo ni vema ukajifunza usiwe mtu wa kuendekeza tamaa za mwili, kiasi kwamba unalazimika kufanya mapenzi popote, wakati wowote hata kwenye nguzo ya umeme ama makaburini ili tu kuuridhisha mwili wako.

KUPOTEZA HAMU YA TENDO (Sexual Dysfunction)
Wapo watu ambao wana pupa za kufanya mapenzi, hawa hupoteza haraka hisia za kimapenzi kwa wapenzi wao kutokana na sababu za kisaikolojia zinazoweza kujitokeza wakati wa kufanya tendo la ndoa mara kwa mara.

Sababu hizo zinaweza kuwa ni pamoja na zile za kumzoea mwenza kiasi cha kukosa msisimko hata anapomuona akiwa mtupu (katika mazingira ya kujumuika katika tendo).

Aidha, kukinai haraka staili za kimapenzi kutokana na kukutana mara kwa mara kwa aina zile zile za mapenzi na pengine sehemu moja, kitanda kimoja na chumba kile kile, jambo ambalo linaweza kumfanya mhusika asione jipya kutoka kwa mwenza wake, hivyo kupoteza mvuto naye na kuhisi kama hawezi tena kushiriki tendo la ndoa kikamilifu.

KUUJAZA MWILI TAMAA KUBWA
Tabia ya kufanya mapenzi mara kwa mara huongeza uzalishaji wa homoni mwilini na kuufanya mwili uwe na msukumo mkubwa wa kutaka kuridhishwa kwa tendo la ndoa bila kukosa na hivyo kumfanya mhusika asiwe mtu mwenye uwezo wa kuzuia tamaa na kukosa chaguo la nani wa kufanya naye mapenzi na kwa wakati gani, yeyote atakayemuona yeye analiswaga twende tu ili afurahie.

Kuna watu wanajiendekeza kufanya mapenzi mara kwa mara, hawa ni wale ambao kila wanayemtazama barabarani humtamani bila kujali hadhi yake, afya yake, background yake, hawa ndiyo wanaobaka, kusaliti ndoa zao hata kwa kutembea na watumishi wao wa ndani au kufanya mapenzi na watoto wao wa kuwazaa, ndugu, watoto wa ndugu n.k kwa vile akili zao huwa zimeathirika kwa tamaa ya mapenzi.

Dk. Rahul Hajare mtafiti wa Taasisi ya Indian Council of Medical Research anasema unapokuwa mtu wa kufanya mapenzi mara kwa mara huwezi kuwa na uwezo wa kuzuia tamaa yako. Mumeo au mkeo akiondoka siku mbili unatamani kuwa hata na houseboy/housegirl ili akuondolee kiu ya penzi.

KUPOTEZA RAHA KAMILI YA TENDO
Raha ya tendo hutegemea sana hisia iliyopandikizwa moyoni mwako kutokana na mapenzi sahihi na kiu ya kufanya mapenzi, hivyo basi ukiwa mtu wa kufanya mapenzi kila mara unaweza kupoteza msisimko wa tendo na kujikuta unapata furaha ambayo haikutoshi kumaliza tamaa yako.

Iwapo ni mapenzi utakuwa unayafanya kwa mazoea tu na msisimko wako utakuwa mdogo (libido).

KUPOTEZA NGUVU ZA MWILI
Madhara mengine yanayoweza kupatikana kwa kufanya mapenzi mara kwa mara ni pamoja na kupoteza nguvu nyingi za mwili. Kama tujuavyo tendo la ndoa hasa kwa wanaume huwafanya watumie nguvu nyingi, hivyo kuufanya mwili uchoke.

Aidha lishe inapokuwa ndogo kwa wafanya mapenzi mwili hukosa nguvu za kutosha kuhimili misukosuko ya kimaisha. Sambamba na hilo mbegu za uzazi zinazotoka kwa wanaume wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa dhaifu.

KUPATA MAGONJWA
Igafamike kwamba watu wanaofanya mapenzi mara kwa mara huwa wana tamaa na hujikuta wanafanya mapenzi holela ambayo huweza kuwasababishia magonjwa ya zinaa yakiwemo magonjwa ya ngono kama ukimwi na mengine.

Dr. Jen Gunter, anasema mwanamke hutengeneza milimita 1–4 za ute wa kurainisha uke kwa siku, hii husaidia wakati wa kufanya tendo la ndoa.

Mapenzi yasiokuwa na msukumo wa kutosha hasa kwa wanawake huwafanya waishiwe msisimko na kuzifanya sehemu zao za siri kutotoa ute unaoweza kuwa kinga na michubuko na maumivu wakati wa tendo la ndoa na hivyo kuwasababishia michubuko itakayoweza kuleta maambukizi ya haraka ya magonjwa ya zinaa ukiwemo ukimwi.

Madhara mengine;
  • Maumivu wakati wa kukojoa (micturition)
  • Uchovu na usingizi kupita kiasi (drowsiness)
  • Misuli ku-paralaizi (dysarthria)
  • Kupoteza kumbukumbuku.
  • Kupata miwasho na mikwaruzo ya ngozi.
  • Kuongezeka/kupungua uzito
  • Kukosa usingizi (insomnia)
  • Matatizo ya misuli.
Ushauri wa bure, ni vema kwa wapenzi kupunguza kiwango cha kufanya mapenzi ili kuifanya miili iwe na uvumilivu unaoweza kumsaidia mtu kukaa kwa muda mrefu bila kumsaliti mpenzi wake hata kama atakuwa amesafiri mbali naye kimasomo, kikazi au kibiashara.

LIKE UKURASA HUU UKITUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK USIPITWE MAKALA NA MENGINE MENGI

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO

KWA TELEGRAM👇BONYEZA HAPA
Read More

Wednesday, May 11, 2022

KUBUSIANA NI ZAIDI YA MSWAKI KIAFYA

May 11, 2022
KUBUSIANA NI ZAIDI YA MSWAKI KIAFYA
DAKTARI bingwa wa meno kutoka nchini Uingereza anasema watu wanapaswa kubusiana dakika 4 kwa siku ili kudumisha afya ya meno, lakini aliongeza kuwa kupigana busu si sawa hata kidogo na kupiga mswaki mara kwa mara na hakuna mbadala wake katika tiba ya afya ya kinywa ukilinganisha na kubigana busu kwa dakika nne mfululizo.

Watu wanapaswa kuongeza kupigana mabusu na kubembelezana kimahaba kwa dakika nne katika utaratibu wao wa kila siku ili kuongeza uzalishaji wa mate na kuosha bakteria wabaya waliokwama kwenye meno yao daktari bingwa alisema.

‘Mate ni muhimu kwa sababu hukusaidia kutafuna, kuonja, kumeza, kupigana na vijidudu mdomoni mwako na kuzuia harufu mbaya ya kinywa – jambo ambalo ni bora wakati wa kubusu.’

Mate pia hupunguza asidi ambayo hukaa kwenye meno yako, na kusaidia kupunguza hatari yako ya kuoza kwa meno.

Kubusu kunaweza kusaidia kuweka sawa afya ya meno yako na kuzuia harufu mbaya ya kinywa, alisema Daktari Khaled Kasem.

LIKE UKURASA HUU UKITUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK USIPITWE MAKALA NA MENGINE MENGI

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO

KWA TELEGRAM👇BONYEZA HAPA
Read More

Tuesday, May 10, 2022

HIZI HAPA SABABU MPYA KWANINI WANAUME HAWAOI

May 10, 2022
HIZI HAPA SABABU MPYA KWANINI WANAUME HAWAOI
Kumekuwa na maswali yasiyo na majibu miongoni mwa jamii kwamba imekuwaje vijana wa kiume wamekuwa ni waongo hasa linapokuja suala la kuoa?

Kwa kadiri siku zinavyokwenda ndivyo ambavyo idadi ya wanaume wanaoogopa kuoa inazidi kuongezeka.

Utakuta wapenzi wanaambiana kwamba wanapendana na kuahidiana kuwa wataoana, lakini kitakachotokea baada ya hapo ni mwanaume kuanza kupiga chenga kwa visingizio lukuki.

Ukweli ni kwamba hakuna jibu la moja kwa moja juu ya tatizo hilo, lakini zipo sababu mpya ambazo walau zinatoa tafakuri;

Ukosefu wa mtu wa kumchukulia kama mfano; hapa nawazungumzia wale watoto wa kiume waliolelewa malezi ya upande mmoja; yaani walilelewa na mama peke yao.

Sina maana ya kudharau au kutweza malezi ya mama, la hasha, lakini ni vyema mkafahamu kwamba kuwa na baba asiye na malezi mazuri si sawa na kutokuwa na baba. Na ndiyo maana nikasema ukosefu wa mtu wa kumchukulia kama mfano.

Achilia mbali aina ya malezi atakayoyapata kwa familia yawe mazuri au mabaya, lakini lazima kutakuwa na tabia za kiume zitakazoakisi malezi ya mtoto wa kiume kwenye familia husika.

Watoto waliolelewa na mama peke yao kuna kitu huwa wanakosa, kwani wanakuwa hawana mtu wa kumchukulia kama mfano kwa upande wa jinsi ya kiume na hapo ndipo hujikuta wakijifunza wenyewe namna ya kuongea na kutenda kama wanaume kwa sababu katika makuzi yao hawakupata fursa ya kuwa karibu na baba zao.

Kwa kuwa siku hizi kuna kundi kubwa la akina mama ambao wamejikuta wakiachiwa mzigo wa malezi ya watoto, baada ya aidha kuachwa na waume zao au kuzalishwa na kutelekezwa (single mothers) na hapo ndipo tunaposhuhudia mtoto wa kiume anapokua kwa umri na kimo huku akiwa hana mtu wa kumuangalia kama mfano wa mume.

Wanaume waliopitia malezi ya aina hii huchelewa kuoa kwani huyaangalia maisha ya ndoa kwa namna ya kujaribu na ndipo hapo wengi huishia kuishi kinyumba na wanawake kwa ajili ya kutaka kujifunza namna ya maisha ya ndoa yanavyotakiwa kuwa na ndiyo sababu huchukua muda mrefu kufanya maamuzi.

Kuna migogoro mingi ya kiuchumi; kuna kundi kubwa la vijana siku hizi hawana ajira au hawana uhakika na kipato. Ukweli ni kwamba hakuna mwanaume atakayependa kujiingiza kwenye ndoa wakati hana kazi au uhakika na kipato chake.

Na hiyo ni kutokana na wanawake wengi siku hizi kuonekana kujali zaidi wanaume wenye uhakika na kipato. Hii misemo ya wanawake ya kebehi dhidi ya wanaume wasio na ajira au kipato, kama vile ‘mwanaume suruali’ ina mchango mkubwa kwenye kuwafanya wanaume kukwepa kuoa kama hawana ajira au hawana uhakika na kipato chao.

Kiwango cha elimu ya juu; siku hizi wanawake wengi wameibuka katika kutafuta elimu ya juu kwa juhudi kubwa. Idadi ya wanawake wanaojiunga na vyuo vikuu ni wengi tofauti na ilivyokuwa zamani. Na hiyo ni kutokana na wazazi wengi kubadili mtazamo wao juu ya mtoto wa kike.

Zamani mtoto wa kike alichukuliwa kama kitega uchumi. Kwa maeneo ya vijijini na katika familia maskini, watoto wa kike walikuwa wanatazamwa kama ‘biashara ya kesho’ ambapo watauzwa kwa njia ya mahari. Kwa hiyo thamani yao ilikuwa ni kuolewa, ni ile ya kibidhaa na siyo kibinadamu.

Lakini tofauti na zamani siku hizi hata vijijini kumekuwa na mwamko mkubwa wa kumsomesha mtoto wa kike hadi elimu ya juu. Kutokana na mwamko huo wanawake wengi wamejikuta wakiona elimu kama kimbilio pekee la kuepukana na mfumo dume.

Wanaume huwaona wanawake kama tishio wanapokuwa na mafanikio makubwa kippesa; inaweza kutokea mwanaume anaweza kuwa na uhusiano na mwanamke ambaye labda tu nisema ni mbangaizaji.

Wakati huo anaweza kuahidi kufunga ndoa na mwanamke huyo, lakini iwapo itatokea mwanamke huyo akapata mafanikio kibiashara na kuinuka kipesa. Kama mwanamke asipokuwa makini anaweza kusababisha mwanaume huyo akaingia mitini. Sababu kubwa hapo inaweza kuwa ni hofu ya kuogopa kuongozwa na mwanamke.

Wanaume wengi siku hizi wana hofu ya majukumu, hasa ya kulea watoto; kutokana na malezi yao au kile wanachokijua kuhusu watoto, baadhi ya vijana huamini kwamba, kulea watoto ni jambo gumu. Lakini wengine wanaamini kwamba, hata mke anapaswa kulelewa kama ilivyo kwa mtoto.

Hivyo wanaamua kutafuta kwanza uwezo ambao haupatikani kirahisi. Kuna wengine, ambao wamefundishwa au kuelekezwa na mila na desturi zao kwamba, kabla hawajaoa, ni lazima wawe na nyumba kwanza, tena kwao. Kwa hiyo, hawa hadi waje wapate uwezo wa kipesa wanakuwa wameshachelewa.

Kuna baadhi ya wanaume, maisha bila ya ndoa wanayaona kuwa ndiyo bora kuliko yale ya ndoa; kuna baadhi ya wanawake hujirahisisha kwa wanaume. Siku hizi ni jambo la kawaida kukuta mwanaume anaishi na mwanamke bila ndoa.

Na hapo ndipo unapokuta wanaume hawaoni tena umuhimu wa kuoa. Sasa kama mwanamke anaweza tu kuishi na mwanaume bila ndoa na mwanaume huyo akapata huduma zote kutoka kwa mwanamke huyo, unadhani ni kitu gani kitamvuta kufunga ndoa?

Jambo lingine ni ile dhana kwamba maana ya ndoa ni tendo la ndoa; Siku hizi wanaume wengi wamejikuta wakiwa hawahitaji tena kuoa kwa sababu tendo hilo linapatikana kirahisi tofauti na zamani. Siku hizi inawezekana kumtongoza binti leo na kupata tendo siku hiyohiyo.

LIKE UKURASA HUU UKITUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK USIPITWE MAKALA NA MENGINE MENGI

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO

KWA TELEGRAM👇BONYEZA HAPA
Read More

Monday, May 9, 2022

FAHAMU FAIDA ZA KULA PARACHICHI KWA AFYA YAKO

May 09, 2022
FAHAMU FAIDA ZA KULA PARACHICHI KWA AFYA YAKO
PARACHICHI
ni miongoni mwa matunda yenye ladha nzuri na ni maarufu hapa Tanzania. Kutokana na utamu na wingi wake wa mafuta, unaweza kudhani siyo tunda zuri kiafya hasa kwa kuwa halina ladha ya sukari lakini ukweli tunda hilo ni msaada mkubwa kiafya.

Tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa watu wenye mazoea ya kula tunda hilo kwa wingi huwa na afya njema na uzito unaokubalika kiafya.

Tunda hilo lenye mafuta mengi, wingi huo unasaidia kupunguza hatari ya mtu kupatwa na kiharusi au ugonjwa wa moyo.

Miongoni mwa faida za parachichi ni pamoja na kudhibiti shinikizo la damu, kushusha kiwango cha lehemu (lower cholesterol levels), kudhibiti ugonjwa wa kisukari, kupunguza maumivu ya viungo na magonjwa ya kuvimba pamoja na kuimarisha uwezo wa kuona vizuri.

Faida nyingine ni pamoja na kuimarisha mifupa ya mwili, kuimarisha usagaji wa chakula tumboni, lakini pia parachichi ni moja ya matunda ambayo hufaa zaidi kuliwa na wajawazito.

Aidha, tunda la parachichi lina virutubisho vya aina mbalimbali, ambavyo ni pamoja na vitamin C, B6, E, K pamoja na madini ya ‘copper’ na ‘potassium.’

Mbali na tunda la parachichi kuwa tiba, pia hata majani ya mparachichi ni tiba ya magonjwa mbalimbali ikiwa ni pamoja na matatizo ya vidonda vya mdomoni na kuimarisha meno na kupunguza maumivu ya meno.

Majani yake yanapochemshwa kama chai na mtu kunywa husaidia kuondoa matatizo mbalimbali mwilini, kama vile hali ya uchovu, udhaifu, kuumwa kichwa, koo, tumbo, mapafu na uvimbe.

Vilevile majani ya mparachichi yana nafasi ya kumsaidia mwanamke ambaye hupata maumivu wakati wa kipindi cha hedhi, ili yatumike katika tatizo hili mhusika atalazimika kupata majani 6 ya mparachichi na kuyachemsha kwenye maji lita moja na kuyaacha yapoe kabla ya kuanza kunywa.

Majani ya mparachichi pia husaidia kutibu majeraha, ili kufanikiwa katika hili unapaswa kusaga majani hayo kisha mhusika atahitajika kutumia unga huo wa majani ya parachichi kwa kuweka sehemu yenye jeraha kila siku kutwa mara tatu.

Majani ya mti wa mparachichi pia husaidia kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali na kumuepusha mhusika kukumbwa na vimelea vya magonjwa.

Pia mbegu ya tunda la parachichi nayo huwasaidai wale wenye shida ya kupata maumivu na kukwama kwa haja ndogo (mkojo). Ili mbegu hiyo ya parachichi iwe tiba ya tatizo hilo ni lazima kwanza isagwe hadi iwe unga kabisa na kisha kukaangwa kidogo. Baada ya zoezi hilo kukamilika mhusika (mgonjwa) atakuwa akitumia unga huo kwa kuchanganya kwenye maji ya moto na kunywa.

Sanjari na faida hizo, bado parachichi linaendelea kuonekana na umuhimu kwa maisha yetu kwani husaidia pia kwenye masuala ya urembo hususan urembo wa ngozi pamoja na kukuza nywele na kuzifanya kukua vizuri bila kukatika.

Mbali na hayo, tunda hilo ni muhimu watoto pia kwani huwasaidia kuwa na ngozi nzuri na kukua vizuri huku wakiwa na afya bora.

Miongoni mwa faida za parachichi kwa mtoto ni pamoja na kumpatia vitamini nyingi pamoja na madini na miongoni mwa vitamin hizo ni pamoja na vitamin C, A, E na vitamin B-6 pamoja na madini kama vile ‘calcium,’ madini ya chuma, ‘magnesium,’ ‘potassium’, ‘zinc’, ‘phosphorous’ na ‘sodium’ ambayo yote hayo ni muhimu sana kwa maendeleo ya afya ya mtoto.

Aidha, matumizi ya tunda la parachichi kwa mtoto husaidia sana kuboresha afya ya macho na akili ya mtoto.

Pia matumizi ya parachichi husaidia kuimarisha mmeng’enyo wa chakula kwa mtoto na hivyo kumuepusha dhidi ya tatizo la kukosa choo, lakini pia husaidia kuondosha maumivu madogomadogo ya tumbo na ili kupata faida zaidi ni nzuri ukapata juisi yake.

Matumizi ya mara kwa mara ya parachichi husaidia kulinda afya ya ini kwa watoto na hivyo kumuepusha dhidi ya magonjwa ya ini pamoja na moyo.

LIKE UKURASA HUU UKITUMIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK USIPITWE MAKALA NA MENGINE MENGI

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO

KWA TELEGRAM👇BONYEZA HAPA
Read More

Thursday, April 14, 2022

MAMBO MUHIMU YA KUFANYA BAADA YA KUMALIZA KUFANYA MAPENZI

April 14, 2022
MAMBO MUHIMU YA KUFANYA BAADA YA KUMALIZA KUFANYA MAPENZI
Wanaume na wanawake walio wengi pindi wanapomaliza kufanya mambo yao na wapenzi wao chumbani hujikuta wakikaa pembeni bila kuzingatia vitu muhimu vinavyotakiwa kufanywa pindi wanapomaliza tendo. 

VIFUATAVYO NI VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA PINDI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO NA MPENZI WAKO CHUMBANI:
1. MFUTE FUTE MPENZI WAKO
Mpenzi msomaji fahamu kuwa unapokwenda kufanya mapenzi na mpenzi wako hakikisha unakwenda ukiwa na kitambaa kisafi (LESO) hiki kitambaa unakuwa nacho maalum kwa ajili ya kumfuta mpenzi wako pindi mnapomaliza kufanya mapenzi.

Hakikisha unapomaliza kufurahia na mpenzi wako unamfuta jasho mwilini na pitisha kitambaa chako katika sehemu zake za siri mfute fute taratibu mpenzi wako usikubali mpenzi wako ajifute yeye mwenyewe na usisubiri akuambie umfute.

2. MUULIZE MPENZI WAKO KAMA KARIDHIKA AU BADO ANAHITAJI KUENDELEA
Wapenzi walio wengi wanapomaliza kufanya mapenzi huwa hawaulizani swali kama hili wengi hujistukia na kuamua kuvaa nguo zao na kuondoka hili ni kosa kubwa, siku zote katika mapenzi mwanaume huwahi kufika kileleni kuliko mwanamke hivyo mwanaume hujikuta ameisharidhika ikiwa mwanamke hajaridhika hivyo ni vizuri pindi unapojiona umeridhika muulize na mpenzi wako kama nae karidhika akikuambia tayari basi mnaweza kuishia hapo au akikwambia bado ni wajibu wako wewe kuendelea tena kufanya mapenzi mpaka nayeye aridhike.

Lakini kuna tatizo moja hujitokeza sana kwa upande wa wanawake, wanawake walio wengi wanapoulizwa na wapenzi wao kama wameridhika huwajibu wapenzi wao "Ndio nimeridhika" lakini kumbe bado hawajaridhika. Napenda niwaambie wanawake wote wenye mtindo huu kuwa si mzuri kuweni wakweli pindi unapoona hujaridhika usimfiche mpenzi wako mwambie ukweli kwani ni haki yako kuridhishwa.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More

Friday, April 8, 2022

DALILI KUU ZA KUJUA KAMA UMEPATA MIMBA

April 08, 2022
DALILI KUU ZA KUJUA KAMA UMEPATA MIMBA
1. Kuwasha na kuvuta kwa chuchu
Kadiri homoni za mimba zinavyoongeza usafirishaji wa wa damu kwenye matiti yako, unaweza kuhisi hali ya kuvuta kuzunguka chuchu zako.

Hii inaweza kuwa moja ya dalili za awali za mimba, na muda mwingine kugundulika pia ndani ya wiki au zaidi ya utungaji wa mimba. Mara baada ya mwili wako kuzoea  ongezeko la homoni, hali hii itapotea.

2. Maumivu ya tumbo na kuona matone ya damu kwenye nguo za ndani.
Sio kawaida kuchafuka ukiwa karibia wiki 6 za ujauzito. Unaweza kugundua rangi ya pinki kwa mbali au madoa ya kahawia katika nguo zako za ndani(chupi) au wakati unakojoa au kuhisi maumivu ya tumbo kwa mbali. Wataalamu hawana uhakika kabisa kwanini dalili hizi zinatokea katika hatua za awali za mimba. Inasadikika ni kwasababu ya ukuaji wa plasenta.

Kama umekumbwa na tatizo la kutokwa damu ambalo sio kawaida, muone daktari mapema ili kuwa katika hali ya usalama.

3. Kujisikia kuumwa
Kama una bahati utaepuka kichefuchefu kabisa. Hata hivyo,magonjwa ya asubuhi ni moja ya dalili za awali za kawaida za mimba, japo zinaweza kuanza mapema katika wiki ya nne.

Unaweza kujisikia kuumwa na kichefuchefu. Hali hii inaweza kukupata mda wowote ndani ya siku, mchana au usiku.

4. Kukua,kuvimba kwa matiti
Mara baada ya kufika wiki ya sita ya ujauzito wako, matiti yako yanakua nyeti zaidi. Inakua sawa na jinsi unavyojisikia kabla ya hedhi.

Unaweza kugundua kwamba maziwa yako yamekua na kuvimba,na mishipa kuonekana chini ya ngozi. Kukua kwa maziwa ni dalili ya kawaida katika miezi mitatu ya kwanza ya mimba.

5. Kujisika kuchoka
Umechoka?Unaweza kushinda kitandani mda wote kadiri mwili wako unavyojitahidi kukubaliana na uwepo wa mtoto ndani yako, tangu mwanzo wa mimba. Homoni za mimba za mwili wako ndio zinakufanya kuhisi umechoka, mwenye hasira na hisia kali.

Uchovu ni dalili ya kawaida ya mimba, na hutokea zaidi katika kipindi cha kwanza cha mimba na hatua za mwisho za ujauzito.

6. Kupata haja ndogo mara kwa mara
Katika wiki yako ya sita ya mimba utagundua unakojoa sana. Hii ni kwasababu ya mjumuiko wa homoni za mimba, wingi wa damu ndani ya mfumo wako na figo zako kufanya kazi nzito zaidi.

Ikiwa utahisi maumivu au kuungua wakati unakojoa, unaweza ukawa na UTI, muone daktari kama unahisi umepata maambukizo ya ugonjwa huu.

7. Chuchu nyeusi
Mabadiliko ya ngozi ni ya kawaida wakati wa ujauzito. Moja ya mabadiliko ya kwanza ambayo unaweza kuona ni mduara wa ngozi pande zote za chuchu zako (vidogo) vinakua nyeusi. Hii inaweza kutokea kutoka wiki nane.

Unaweza pia kupata kwamba  vifungo vidogo vyangozi  vinavyozunguka chuchu zako vinajitokeza zaidi na kuchomoza zaidi. Vumbu yako na uke hubadilika na kua nyekundu zambarau iliyokolea, ingawa unaweza usione hili.

8. Hamu ya kula kubadilika na hata hisia ya harufu hubadilika
Mabadiliko katika matamanio ya chakula yanaweza kuwa dalili ya ujauzito. Unawezekana kuacha ladha fulani wakati wa kwanza, hasa kabla hujakosa kuona hedhi yako. Unaweza kuhisi ladha ya chuma katika kinywa chako, au kushindwa kutumia kahawa yako ya asubuhi au chakula ambacho unachokipenda, kama vile mayai.

Hisia yako ya harufu inaweza pia kubadilika, mabadiliko haya yanaweza kuwa makali zaidi kwenye chakula na harufu ya mapishi.

Hamu ya kula inaweza ikawa ni moja ya dalili za mimba/ujauzito. Unaweza kuachana na aina fulani za chakula mwanzoni hata kabla hujakosa siku zako.

Utaanza kutambua hisia ya chuma mdomoni, au kutambua hupati hamu ya kunywa ya kahawa, au chakula ambacho umezoea kula.

9. Kukosa hedhi
Ikiwa hedhi yako ni ya kawaida, na hedhi yako haijaanza kwa muda, ni bora ukachukua kipimo cha mimba kabla hujagundua dalili nyingine. Kukosa hedhi yako ni moja ya ishara hakika ya ujauzito. Lakini ikiwa  hedhi yako si ya kawaida au unapoteza dira ya hedhi ijayo inakuja lini, unaweza usigundue kama hedhi yako imechelewa.

Katika kesi hiyo, matiti ya kukua, hisia za kichefuchefu na kufanya safari za ziada chooni inaweza kuwa dalili za mwanzo kuwa wewe ni mjamzito.

10. Kipimo cha nyumbani cha mimba
Vipimo vingi vya mimba vya nyumbani vitakupatia majibu ya uhakika , kama ukisubiri mpaka siku ya kwanza ya kukosa hedhi yako.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More

Wednesday, April 6, 2022

ZITAMBUE SIRI AMBAZO MWANAMKE KAMWE HAUPASWI KUMWAMBIA MUMEO

April 06, 2022
ZITAMBUE SIRI AMBAZO MWANAMKE KAMWE HAUPASWI KUMWAMBIA MUMEO
NDOA ni muhimu, na huwa muhimu kwasababu ni kitu kinachowaunganisha mume na mke na kuanzisha familia, na huleta baraka nyingi kama vile watoto na nyinginezo nyingi.

Hata hivyo siku hizi, ndoa nyingi huishia kuvunjika kutokana na sababu moja au nyingine, hususani kutokana na ugomvi ndani baina ya wanandoa.

Bila shaka haipaswi kuwa siri baina ya wanandoa, lakini kuna baadhi ya vitu ambavyo mwanamke hapaswi kumwambia mume wake, hata kama wanapendana kiasi gani.

Katika jamii nyingi za kiafrika kuna msemo usemao, maskio yasiposikia, moyo hauwezi kukasirika. Na kama tunataka amani ndani ya familia lazima kutakuwa na matukio magumu, na mwanamke anapaswa kusaidia katika utatuzi wa mambo hayo.

Yafuatayo ni mambo 5 ambayo mwanamke hapaswi kumwambia mume wake:
1. Idadi ya wanaume uliojamiana nao kabla ya kuoana na mume wako
Haupaswi kumfahamisha mpenzi wako wa kiume au mume wako ni wanaume wangapi ulikutana nao kimwili kabla ya kuishi naye.

Swababu ni kwamba unaweza kufikiri hautamkosea mume wako siku sijazo. Na kama idadi ya wanaume uliyomwambia ni wengi anaweza kufikiri wewe ni kahaba au mzinzi.

Kwahiyo, iwapo atakuuliza ni wanaume wangapi ulishawahi kukutana nao kimwili, unaweza kucheka tu na umwambie: ”Ebu wacha tuachane na hayo, lakini swala la ni wangapi halihusiani na safari ya mapenzi. Hebu njoo...“.

2. Kusema siri za mpenzi wako wa kiume au mume wako wakati mmoja
Ukiulizwa maswali kumuhusu mwanaume, mujibu machache. Usiseme mambo ambayo yanaweza kumfanya mume au mpenzi wako ahisi kwamba sio bora vya kutosha, au ajihisi kuwa mtu mbaya.

Usizungumzie kuhusu -ungependa kuwa na uhusiano na mwanaume tajiri kiasi fulani, mwenye uwezo wa kingono kiasi gani, na ni kwa vipi ungependa ampende mke wake, kwa mume mpya.

3. Usimwambie mume wako kwamba unampenda sana rafiki yako au shemeji yako
Sote tunafahamu kuwa inawezekana kwa rafiki au shemeji kutaka kukuoa. Lakini, ni hatari kumwambia mume wako kuhusu wazo hili. Sababu ni kwamba mume wako anaweza kuanza kuwa na mashaka kuhusu tabia zake na vitendo vyako kumuhusu mwanaume huyo, jambo linaloweza kusambaratisha ndoa yako.

4. Usijaribu kumwambia kuwa unamchukia mama yake au familia yake
Hata mama mkwe awe ni mtu nmbaya kiasi gani, usimwambie mume wako kuwa unamchukia. Au unaichukia familia yake. Hata kama umekasirika kiasi gani, usijaribu kusema mambo mabaya kuwahusu, au kumuona mume wako sawa na familia yake.

Kama haupatani na yeyote katika familia ya mume wako, elezea kwa utulivu, ukiwa na matumaini kuwa ataelewa ni kwanini haupatani nao.

Mume wako pia ataweza kukusaidia kutatua tatizo, na pia itazuia matatizo mengine ambayo yanaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi.

5. Usimtishe mume wako kuwa utakuja kutalikiana naye
Siku utakapomwambia mume wako kuwa utaachana naye wakati mnazozana, jua ndio mwanzo wa malumbano ndani ya ndoa. Ndoa itaanza kukumbwa na misukosuko, wasi wasi na kutoamianiana.

Kutishia talaka katika ndoa inamaanisha kuwa hauna moyo wa imani katika ndoa, na haupatii umuhimu. Isipokuwa kama katika ndoa kuna unyanyasaji au uhalifu mwingine mbaya, ni vyema kujaribu kushirikiana kutatua changamoto zozote mlizonazo.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More

Thursday, January 6, 2022

CHANZO, DALILI NA TIBA YA TATIZO LA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI

January 06, 2022
CHANZO, DALILI NA TIBA YA TATIZO LA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI
Tatizo la kuziba mirija ya uzazi ni tatizo ambalo hutokea kwa wanawake wengi kwa hivi sasa, na ni miongoni mwa sababu kubwa za wanawake wengi kushindwa kubeba Mimba.

Je tatizo hili la kuziba kwa mirija ya uzazi chanzo chake ni nini? soma hapa chini kufahamu baadhi ya sababu zinazochangia kutokea kwa tatizo hili la kuziba kwa mirija ya Uzazi.

CHANZO CHA TATIZO LA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI NI PAMOJA NA;
  • Mwanamke kuwa na historia ya kupatwa na maambukizi kwenye via vyake vya uzazi mara kwa mara yaani pelvic inflammatory disease(PID)
  • Mwanamke kuwa na historia ya kuumwa na kidole tumbo yaani Appendix kisha ikapasukia ndani
  • Mwanamke kuwa na maambukizi ya magonjwa ya zinaa(Sexual transmitted diseases-STD’s) kama vile; Ugonjwa wa kisonono(gonorrhea),tatizo la chlamydia n.k
  • Tatizo la Endometriosis, ambapo huhusisha kukua kwa kuta za ndani ya tumbo la uzazi kuelekea nje
  • Mwanamke kuwa na historia ya kufanyiwa upasuaji tumboni
  • Mwanamke kupatwa na tatizo la maji kujaa kwenye mirija ya uzazi kisha kusababisha mirija ya uzazi kuziba na kuvimba, tatizo ambalo kwa kitaalam hujulikana kama Hydrosalpinx
  • Mwanamke kuwa na historia ya kupatwa na tatizo la mimba kutunga nje ya kizazi yaani Ectopic pregnancy
  • Mwanamke kuwa na tatizo la uvimbe kwenye mirija ya uzazi yaani Fibroids n.k
DALILI ZA TATIZO HILI LA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI
Kwa asilimia kubwa wanawake wengi wenye tatizo hili la kuziba mirija ya uzazi hawaonyeshi dalili zozote, mpaka pale watakapoanza kupata shida ya kutokubeba mimba, ndipo huamua kufanya vipimo na kugundulika shida hii, Lakini endapo watapata dalili, basi miongoni mwa dalili hizi hapa chini huweza kuonekana;
  • Mwanamke kupata maumivu makali ya tumbo eneo la kwenye kitovu, chini ya kitovu, pembeni upande mmoja au kwenye kiuno
  • Mwanamke kupata maumivu makali sana wakati wa hedhi
  • Mwanamke kupata maumivu ya tumbo upande mmoja, hii hutokea sana kwa wanawake ambao tatizo la mirija ya uzazi kuziba chanzo chake ni maji kujaa na kuziba kwenye mirija ambapo kwa kitaalam hujulikana kama Hdyrosalpinx
  • Baadhi ya wanawake hupata shida ya kutoa damu ukeni yaani vaginal bleeding n.k
MADHARA YA TATIZO HILI LA MIRIJA YA UZAZI KUZIBA
✓ Kwanza ifahamike kwamba, mwanamke huweza kupata shida ya mirija ya uzazi kuziba upande mmoja au mirija yote miwili yaani kulia na kushoto

Endapo kuziba kumetokea upande mmoja uwezekano wa mwanamke huyu kubeba mimba bado upo, ila Mwanamke huyu yupo pia kwenye hatari ya mimba hii kutunga nje ya kizazi, yaani kupatwa na tatizo la Ectopic pregnancy

Na endapo mirija yote miwili ya Uzazi imeziba ningumu sana kwa mwanamke huyu kubeba mimba mpaka atibiwe

VIPIMO AMBAVYO HUWEZA KUFANYIKA
Moja ya vipimo ambavyo huweza kufanyika ni pamoja na;
  1. Kipimo cha Hysterosalpingograph(HSG), Kipimo hiki ni aina ya X-ray ambayo husaidia kuona ndani ya mirija ya uzazi
  2. Na kipimo kingine ni Laparoscopy N.k
MATIBABU YA TATIZO LA KUZIBA MIRIJA YA UZAZI
Moja ya tiba kwenye tatizo hili ni pamoja na Mwanamke kufanyiwa upasuaji wa kuondoa uvimbe, kuondoa Scars, au huduma ya Kuzibua mirija n.k Kutegemea na chanzo cha tatizo lenyewe.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More

Saturday, January 1, 2022

JINSI YA KUNYONYA MATITI YA MWANAMKE MPAKA AKOJOE

January 01, 2022
JINSI YA KUNYONYA MATITI YA MWANAMKE MPAKA AKOJOE
Mara nyingi maziwa ni sehemu ambayo huwa na hisia sana kwa mwanamke endapo itanyonywa vizuri, wengi hawajui namna ya kunyonya maziwa ya mwanamke na kama utamnyonya vizuri itatosha kumridhisha mwanamke bila ya kumfanya.

Zifuatazo ni dondoo muhimu wakati unamnyonya mwanamke maziwa:
  1. Anza kwa kuliramba titi lotee huku unalipaka mate taratibuu, kama una ulimi mrefu kama mimi basi ni fursa nzitoo na nzuri kuugusisha ulimi wako katika kila kona ya ziwa, hapo utamuona mwananmke anaanza kujinyonga nyonga kwa rahaaa
  2. Lishike ziwa kwa mkono wako na hapo anza kunyonya sehemu ya juu ya maungio ya mwili na ziwa, hiyo ni sehemu ambayo ina nyege sana na hapo pekee panatosha kumkojoza mwanamke ikiwa utatumia ulimi wako vizuri
  3. Lishike ziwa tena na linyonye katika sehemu ya chini ambayo ni kama uvungu wa ziwa, hapo ni sehemu ambayo nerves zimepita kwahiyo ukiwa unamnyonya utaona mwanamke anatoa ute katika uke ishara ya kuwa yuko tayari kupokea mashine
  4. Chuchu, hii ndiyo sehemu kuu ya ziwa. kwanza hapa ina unyonywaji wa aina tatu
    • Moja, kwanza irambe kwa utaratibi huku kama vile unaimung'unya kama pipi hapo pekee itatosha kumtoa mwanamke mkojo
    • Mbili, ifanye kama unataka kuing'ata chuchu ya ziwa la mwanamke huku unabinya binya ziwa la upande mwengine kwa ustadi mkubwa
    • Tatu, ile chuchu ifanye kama vile unairamba kama koni huku unamsugua taratibu katika ziwa jingine
    • Jambo kubwa jingine ni namna ya kuichezea chuchu kwa mkono, hapo utafanya ifuatavyo: pakaza mate vidole vya mkono wako halafu isugue chuchu kwa madahaa hapo huyo mwanamke ni llazima atafurahia mapenzi yako.
AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More

Thursday, December 30, 2021

VITU HATARI KWA MAMA MJAMZITO

December 30, 2021
VITU HATARI KWA MAMA MJAMZITO
WATAALAMU wa afya wanasema ili mwili ukue vizuri unahitaji vyakula vya aina tofauti tofauti. Iwapo una mtoto, mwili wake unahitaji virutubisho ili kusaidia ukuaji. Kama ni kijana mwili wake una mahitaji maalumu ili kukuza afya vizuri kuelekea utu uzima. Hii ni kwa sababu anapoelekea utu uzima anahitaji kuwa na uzito unaolingana na mwili wake. Kwa upande wa wajawazito na wanaonyonyesha nao wana vyakula vyao maalumu wanavyohitajika tofauti kabisa na wanawake wasio na mimba.

Uchunguzi mmoja uliofanywa kuhusu tiba unaonyesha kuwa, hali ya kiafya ya mjamzito huwa na athari mbalimbali kwa mtoto atakayezaliwa kama mama hatapata lishe bora. Si hivyo tu bali kuna ushahidi mkubwa kuwa magonjwa sugu ya watu wazima huanzia wakati mtoto akiwa bado tumboni mwa mama akiwa katika hali ya kiluilui au kitaalumu foetus.

Kwa hivyo, wajawazito wanashauriwa kuzingatia vyakula wanavyokula kabla na baada ya kushika mimba. Sasa tuangalie athari za chakula kwa afya ya mtoto na virutubisho vinavyopaswa kujumuishwa katika mlo wa mjamzito. Chakula cha mjamzito kinaweza kuwa na athari kubwa kwa afya ya watoto kwa miaka mingi baada ya kuzaliwa.

Miaka kadhaa ya hivi karibuni, Jarida la Masuala ya Lishe la Uingereza la Prestigious lilichapisha makala tatu kuhusu athari za lishe ya mama mjamzito kwa afya na ukuaji wa kiakili wa mtoto ambaye bado hajazaliwa. Wengi wanafahamu kuwa wajawazito wanapaswa kula chakula chenye virutubisho vyote vinavyohitajika ili kuhakikisha watoto wao watakaowazaa wamerutubika vya kutosha wakati wakiwa kwenye fuko la uzazi tumboni.

Hata hivyo, kile ambacho hatukubaliani nacho hivi sasa ni kwamba chakula cha mama mwenye mimba kinaweza kuwa na taathira (matokeo) chanya kwa afya ya watoto kwa muda wa miaka mingi, baada ya kuzaliwa mtoto.

Hivi sasa imethibitika kuwa kile kinacholiwa na akina mama wakati wa ujauzito, chakula ambacho kitakuwa kimejumuisha virutubisho vyote vinavyotakiwa, kama vile cha nafaka zisizokobolewa na matunda, kinaweza kuwafanya watoto wao watakaozaliwa kuwa werevu zaidi. Siku hizi unaweza kuandaa kizazi kipya cha watoto werevu kwa kula chakula kinachotakiwa wakati wa ujauzito.

Wajawazito ambao katika kipindi cha ujauzito hawakupata lishe bora isiyo na protini, nishati, madini na vitamini kwa ujumla huzaa watoto walio na uzito wa chini. Aidha, watoto hao huwa
na uwezekano mkubwa wa kupata magonjwa ya kisukari kipindi cha utu uzima.

MADHARA YA POMBE
Baada ya kufahamu umuhimu wa kula lishe bora kwa mama mjamzito na athari zake chanya kwa mtoto atakayezaliwa, sasa tuangalie hatari ya unywaji pombe kwa wajawazito. Watu wengi wanafahamu madhara yanayotokana na utumiaji wa dawa za kulevya na dawa za kawaida pamoja na uvutaji sigara wakati wa ujauzito, lakini wanawake wengi hawana ufahamu wa kutosha kuhusu madhara yanayosababishwa na unywaji wa pombe wakati wa ujauzito.

Unywaji pombe wa aina zozote wakati mama akiwa na mimba huwa na madhara tofauti kwa mtoto aliye tumboni mwake, kuanzia zile za wastani hadi kubwa. Kuna madhara makuu matatu yanayoweza kumsibu mtoto ambaye bado hajazaliwa iwapo mama yake alikuwa akinywa pombe wakati wa ujauzito.

Mosi, ni kuweko hatari kubwa ya kutoka mimba au kuzaliwa mtoto kabla ya miezi tisa, pili, chembe za mwili za mtoto aliye tumboni zinaweza kuathiriwa au anaweza kuwa na uzito mdogo na kuzaliwa akiwa na ulemavu zaidi ya mmoja. Tatu, chembe za ubongo wa mtoto huyo zinaweza kuharibiwa na pombe na mtoto kuzaliwa akiwa na matatizo ambayo kitaalamu hujulikana kama foetal alcohol syndrome.

Miongoni mwa madhara yanayoweza kumpata mtoto ni kama vile kuzaliwa akiwa na ulemavu wa kimwili na kiakili. Kwa upande wa kimwili, mtoto huweza kuathiriwa na mtindio wa ubongo au brain retardation, mtoto anaweza kuzaliwa akiwa na kichwa kidogo sana, na uso wake kuwa na mwanya mkubwa baina ya pua na mdomo.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More

Sunday, December 26, 2021

JINSI YA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI

December 26, 2021
JINSI YA KUMFIKISHA MWANAMKE KILELENI
Karibuni katika somo jingine ndugu wapenzi, kumekuwa na maombi kwamba nitoe somo kuhusu hili, kama hauwezi kumfikisha mwanamke kileleni basi unahusika katika hili somo!!!!...Wengi wakitaka kujua ni namna gani ya kumfikisha mwanamke kileleni kwa kuzani hawana nguvu za kuhimiri kufanya tendo kwa muda mrefu bila kufikiri kuwa kumuandaa mwanamke kabla ya tendo kunaweza kukusaidia katika kumridhisha.

Wanaume wengi huwa hawana maandalizi mazuri kwa wanawake wao kabla ya tendo la ndoa yanayoweza kuwasaidia kama kichochezi cha kuwafikisha kileleni mapema.

Basi njia hizi zinaweza kuwa msaada mkubwa endapo zitatumika ipasavyo na hata yule ambaye ulikuwa haumridhishi baada ya somo hili utaweza kumridhisha ipasavyo kwa kumfanyia yafuatayo:
  1. Mpe maneno matamu ukimtomasa kwa ulimi sikio lake kimahaba zaidi
  2. Pitisha ulimi wako shingoni kifuani, tumboni, mapajani ni ikibidi zama chumvini walau kwa dakika kumi hivi
  3. Tumia ulimi wako ipasavyo kutomasa kitovu chake
  4. Mnyonye lita kadhaa za mate na huku ukitumia ulimi wako ipasavyo kuuchanganya ulimi wake
  5. Papasa matiti yake huku ukifinya finya chuchu zake na peleka mdomo wako huku ukinyonya kama mtoto
  6. Zungusha viganja vyako karibu kila kona ya mwili wake bila kusahau kubinya binya sehemu za mbavu hips na makalio yake
  7. Chezea ki**mi chake kwa vidole vyako au kwa ulimi ikiwezekana
  8. Mpe koni ya asili ajilambie kwa raha zake
  9. Muweke mkao mzuri wa kupokea zawadi yake
  10. Ingiza taratibu mti shimoni
Hata kama hauna uwezo wa kumfkisha kileleni hiyo dozi itakusaidia vilivyo.

Naamini kama utayafanyia kazi ipasavyo tatizo la kumridhisha mwanamke litapungua..

ZINGATIA YAFUATAYO
Maandalizi kwanza:
Tumia muda wa kutosha mwanzoni, wanawake wanapenda kuingiliwa taratibu bila pupa. Mbusu, mfanyie masaji na mchezee kwa muda, huku ukimnon'goneza maneno machafu masikioni, na tumia muda kumpapasa sehemu nyeti. Anahitaji kuloana hata kabla hujamvua nguo.

Mtafutie Style anayoipenda:
Najua wengi mnapenda ile ya kumuweka juu huku ukimshika matiti yake na makalio. Itunze hiyo utaitumia baadae, mwanzoni jaribu kutafuta style ambayo inamchanganya na kumfurahisha yeye kwanza, kama vipi muulize kwanza.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More

VYAKULA VYA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME

December 26, 2021
VYAKULA VYA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME
Katika ulimwengu wa leo kuna wimbi kubwa la tatizo la upungufu wa nguvu za kiume, kitu ambacho hufikia mahali kuwakosesha raha na amani wanaume walio wengi kwa kuwa wanashindwa kukidhi haja za wenzi wao kwa uhakika na kubaki na msongo.

Tunapozungumzia upungufu wa nguvu za kiume tunamanisha kutokuwa na uwezo wa kufanya kabisa tendo la ndoa(uume kusimama), uume kusimama muda mfupi baada ya tendo la kuanza unasinyaa, na kushindwa kufika mwisho ama kuwahi kufika kileleni.

Mtalaamu wa tiba lishe Amani Ezekiel kutoka kituo cha Focus About Tommorow kilichopo Mkuyuni jijini Mwanza anaelezea kwa undani zaidi juu ya tatizo hili la upungufu juu ya nguvu za kiume na jinsi ya kuepukana nalo.

Mtalaamu huyo anasema kuwa katika tendo la ndoa kwa mwanaume, mishipa ya damu ya ateri ina nafasi kubwa sana sababu ya kazi yake ya usafirishaji wa damu kwenda sehemu mbalimbali za mwili, hivyo unashauriwa kujifunza namna ya kutunza ateri za mwili wako ili kuruhusu mtiririko mzuri wa damu mwilini mwako.

“Katika kujitibu tatizo hili la upungufu wa nguvu za kiume jambo la kwanza ni kuelewa ni nini kimesababisha tatizo hilo kwa upande wako ndipo utaweza kupata matibabu kwa urahisi hata kwa njia ya yakula vyakula tu” alifafanua mtalaamu huyo.

Akiendelea kufafanua juu ya njia zitakazo kufanya uepukane na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume ni pamoja na kuachana na mawazo. ”Mawazo na mfadhaiko huondoa mtiririko mzuri wa damu kwenda kwenye uume na kusababisha kupungua nguvu za kiume na hata uume wenyewe kusinyaa” alifafanua.

Pia anasema ikiwa unasumbuliwa na mfadhaiko(stress) uangalifu mkubwa unahitajika kabla ya kuamua kutumia dawa yoyote. Katika hali ya mfadhaiko wa akili utokanao na hali ya kushuka kwa uchumi kwa mfano, wanandoa wanapaswa kuwa ni wenye umoja na kujaliana zaidi, kwa kutiana moyo na sio kukatishana tama, kwa kutangaza kwa majirani.

Akiendelea kufafanua anasema kuwa kama tatizo limesababishwa na magonjwa kama kisukari, vidonda vya tumbo, shinikizo la juu la damu au uzito kupita kiasi ni vyema ukajitibu kwanza maradhi haya kwa kuwa yanatibika.

“Kisukari, shinikizo la juu la damu, vidonda vya tumbo na hata uzito kupita kiasi ni magonjwa yanayotibika kabisa hasa kwa kutumia dawa mbadala na kufuata muongozo sahihi katika kula na kunywa kwa kipindi cha majuma kadhaa” alifafanua.

Anasema jambo lingine ni kama tatizo linatokana na matumizi ya vilevi, hatua ya kwanza ni kuviacha kwanza hivyo vilevi. Ndiyo kuviacha kwanza, unatakiwa ujiulize mwenyewe kipi ni mhimu kwako ndoa yako au hivyo vilevi? Mtu anayejali vilevi kuliko hata afya yake hafai ni mtumwa wa nafsi.

“Kuna watu wanajidanganya kwamba ukitumia sijuwi kilevi fulani nguvu zinaongezeka, ni kweli zitaongezeka hapo mwanzoni mwa matumizi ya hicho kilevi lakini kadri siku zinavyoenda ndivyo utakavyoendelea kuwa mtegemezi wa hicho kilevi na itafika siku hata hicho kilevi hakitasaidia kitu na hapo ndipo hatari zaidi ya kutotibika tatizo lako itakapojitokeza” anafafanua mtalamu.

Pia kuzingatia kufanya mazoezi ya viungo kumetajwa na mtalamu kama moja ya njia nzuri ya kuepukana na matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume, bila kujishughulisha na mazoezi ya viungo kila siku itakuwa ni vigumu sana kwako kupona tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

“Kutengeneza mishipa na kupunguza uzito isiwe ndiyo sababu pekee ya kwenda gym. Kama unahitaji nguvu za kiume na uume wenye afya, unahitaji kujishughulisha na mazoezi ya viungo mara kwa mara ili kusafisha mishipa ya damu na hivyo kuongeza kiasi cha utiririkaji wa damu kwenda kwenye uume” anafafanua.

Vipo baadhi ya vyakula muhimu kwa kuondokana na tatizo hili, matalamu Ezekiel anasema chukuwa punje 6 za kitunguu swaumu, menya na uzikate vipande vidogo vidogo kisha meza na maji vikombe 2 kutwa mara 1 kwa mwezi mmoja.

Sifa kuu zinazokifanya kitunguu swaumu kuwa na uwezo na faida nyingi mwilini ni kule kuwa kwake na viasili kadhaa(ingredients) ambavyo vinafanya kazi tofauti tofauti. Uwezo wake wa kiutendaji unatokana na sifa zifuatazo:

“Vina uwezo wa kusababisha kutanuka kwa mishipa ya damu(vasodilation) kwa kubadilisha polysulfides zilizopo ndani yake kuwa hydrogen sulfides kwenye seli nyekundu za damu” anafafanua.

Anasema ukivikata vipande vidogo vidogo hivi(chop), vitunguu swaumu hutoa kemikali iitwayo kwa kitaalamu kama ‘Allicin’ ambayo ni dawa dhidi ya bakteria, na ‘Phytoncide’ ambayo huua fangasi mbalimbali mwilinina kufanya nguvu kuongezeka.

Pia anafafanua ulaji wa tikiti maji, tunda hili lina faida nyingi pamoja na kuwa ni chanzo kikuu cha Protini, Mafuta, Nyuzinyuzi, Wanga, Calcium, Phosphorus, Chuma, Vitamin A,B,C, potasium, Magnesium, Carotene, na Anthocyanins.

Tunda linasaidia kuwa na uwezo mkubwa wa kuimalika kwa misuli na mfumo wa fahamu kufanya kazi zake vizuri na kuondoa katika hatari ya kupata shinikizo la juu la damu ambalo linafanya kupungukiwa nguvu za kiume.

“Kula tikiti maji kila siku huku ukitafuna na zile mbegu zake, fanya hivi mara kwa mara kunafanya damu kutiririka vizuri mwilini na kufanya kufika katika uume kwa urahisi na kuondokana na tatizo la upungufu wa nguvu za kiume”

Pia moja ya madaktari wa tiba lishe Raphael Nyampiga kutoka kliniki ya Atukuzwe iliyoko Pugu jijini Dar es Salaam kwa kukazia maelezo hayo aliongezea kuwa, kula ugali wa dona kila siku ni mhimu, kuachana na mazoea ya kula ugali uliokobolewa kwani kuna virutubisho muhimu ndani yake vinavyoamsha hisia za mwanaume na kumuongezea nguvu ya tendo wakati wa tendo.

“Dona ni muhimu mwilini kwa mwanaume na sambamba na matumizi ya chumvi ya mawe ya baharini ile ambayo haijasafishwa au haijapita kiwandani ina mchango mkubwa sana katika kutibu tatizo hili kwa kutumia kila siku katika milo” alifafanua Dk. Nyampiga.

Anaendelea kufafanua mtalamu huyu kuwa kunywa maji ya kutosha kila siku bila kusubiri kiu. Kila mtu anahitaji glasi 8 mpaka 10 za maji kila siku kwa kuwa maji ni muhimu katika kuongeza damu, kusafisha mwili na kuondoa sumu mwilini.

Anaendelea kufafanua juu ya matumizi ya mbegu za maboga, Maajabu mengine ya mbegu za maboga ambayo Dk. Nyampiga anasema na ulikuwa huyajuwi bado ni kuondoa tatizo la upungufu wa nguvu za kiume.

“Kwanza kabisa zinaondoa msongo wa mawazo/stress kitu ambacho ni namba 1 katika kusababisha upungufu wa nguvu za kiume, lakini pia zinashusha lehemu(cholesterol), zinatibu kisukari, zinatibu tezi dume(matatizo kama ya ngiri nk), zina protini nyingi ya kutosha na yenye ubora na mbaya kuliko zote ni kuwa zina madini ya ZINKI madini mhimu kuliko kitu kingine chochote kwenye upande wa nguvu za kiume na kinga ya mwili” ni amelezo yaliyotajwa na watalaamu.

Anasema kuwa Unaweza kula zikiwa kavu na ndiyo utapata faida nyingi zaidi ingawa mimi napenda kuzikaanga kidogo kama dakika 5 hivi na huwa nazichanganya na maji ya chumvi ya mawe ya baharini kidogo kwa mbali ili kupata radha.

“Unahitaji ujazo wa kiganja kimoja cha mkono wako cha mbegu za maboga, ujazo wa kama nusu kikombe cha chai hivi kila siku kwa muda wa wiki 3 mpaka 4, Unatafuna na ganda lake hasa kama zimekaangwa tayari” alifafanua daktari.

Mtalaamu Ezekiel anasema kuwa tumia asali yenye mdalasini, Chukuwa lita moja ya asali safi ya asili ambayo haijachakachuliwa, ongeza vijiko vikubwa 8 vya mdalasini ya unga changanya vizuri pamoja. Acha ndani ya bakuli kubwa ili iwe rahisi kuikoroga vizuri kila unapoitumia. Lamba vijiko vikubwa vitatu kila unapoenda kulala. Fanya hivi kwa mwezi mmoja.

Anasema hata baada ya mwezi mmoja kuisha bado nakushauri uendelee kuitumia asali hivi maisha yako yote au hakikisha haipiti siku bila kunywa au kula chakula chenye asali yenye mdalasini ndani yake.

Pia anasema kuwa ulaji wa tangawizi mbichi nusu saa kabla ya tendo la ndoa husaidia katika kuongeza hamu na nguvu ya tendo la ndoa. Unaweza ukanywa chai ya tangawizi tu nusu saa kabla ya kuanza tendo au unaweza ukatafuna kipande cha tangawizi mbichi kwa ukubwa wa dole gumba la mtu mzima nusu saa kabla ya tendo.

“Kunywa chai ya tangawizi mbichi kila siku, katika chai hiyo unayopika ndani yake weka tu maji na Tangawizi mbichi uliyosagia ndani yake(usiongeze majani ya chai humo), kumbuka tangawizi inaoshwa tu na maji na uisagie ndani ya sufuria pamoja na ganda lake la nje. Sasa badala ya kutumia sukari wewe tumia asali kwenye hii chai yako ya tangawizi na ukiitumia hivi kila siku hutachelewa kuona faida zake” anaeleza mtalaamu Ezekiel.

Kwa ushauri wa kitalaamu ni mhimu sana kuwaona wataalamu wa tiba kuhusu unavyojisikia na jinsi unavyohisi kuwa pengine unaweza kuwa na tatizo katika mishipa yako ya ateri.

Jaribu kujiwekea utaratibu wa kujichunguza afya yako mara kwa mara kama utahisi kunyemelewa na tatizo hili, baadhi ya watu hufanya maradhi kuwa sugu kwa sababu ya kuacha kujichunguza mara kwa mara hadi waugue.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger
Read More