MAMBO MUHIMU YA KUFANYA BAADA YA KUMALIZA KUFANYA MAPENZI - Fabiani 255

Fabiani 255

Jisomee Makala za Afya na Mapenzi Kila Siku

Thursday, April 14, 2022

MAMBO MUHIMU YA KUFANYA BAADA YA KUMALIZA KUFANYA MAPENZI

Wanaume na wanawake walio wengi pindi wanapomaliza kufanya mambo yao na wapenzi wao chumbani hujikuta wakikaa pembeni bila kuzingatia vitu muhimu vinavyotakiwa kufanywa pindi wanapomaliza tendo. 

VIFUATAVYO NI VITU MUHIMU VYA KUZINGATIA PINDI UNAPOMALIZA KUFANYA TENDO NA MPENZI WAKO CHUMBANI:
1. MFUTE FUTE MPENZI WAKO
Mpenzi msomaji fahamu kuwa unapokwenda kufanya mapenzi na mpenzi wako hakikisha unakwenda ukiwa na kitambaa kisafi (LESO) hiki kitambaa unakuwa nacho maalum kwa ajili ya kumfuta mpenzi wako pindi mnapomaliza kufanya mapenzi.

Hakikisha unapomaliza kufurahia na mpenzi wako unamfuta jasho mwilini na pitisha kitambaa chako katika sehemu zake za siri mfute fute taratibu mpenzi wako usikubali mpenzi wako ajifute yeye mwenyewe na usisubiri akuambie umfute.

2. MUULIZE MPENZI WAKO KAMA KARIDHIKA AU BADO ANAHITAJI KUENDELEA
Wapenzi walio wengi wanapomaliza kufanya mapenzi huwa hawaulizani swali kama hili wengi hujistukia na kuamua kuvaa nguo zao na kuondoka hili ni kosa kubwa, siku zote katika mapenzi mwanaume huwahi kufika kileleni kuliko mwanamke hivyo mwanaume hujikuta ameisharidhika ikiwa mwanamke hajaridhika hivyo ni vizuri pindi unapojiona umeridhika muulize na mpenzi wako kama nae karidhika akikuambia tayari basi mnaweza kuishia hapo au akikwambia bado ni wajibu wako wewe kuendelea tena kufanya mapenzi mpaka nayeye aridhike.

Lakini kuna tatizo moja hujitokeza sana kwa upande wa wanawake, wanawake walio wengi wanapoulizwa na wapenzi wao kama wameridhika huwajibu wapenzi wao "Ndio nimeridhika" lakini kumbe bado hawajaridhika. Napenda niwaambie wanawake wote wenye mtindo huu kuwa si mzuri kuweni wakweli pindi unapoona hujaridhika usimfiche mpenzi wako mwambie ukweli kwani ni haki yako kuridhishwa.

AHSANTE KWA MUDA WAKO, NAOMBA SAPOTI KAZI YANGU KWA KUTAZAMA VIDEO HII MPAKA MWISHO
KWA MAONI NA USHAURI NIANDIKIE HAPA
Inbox: Messanger

No comments:

Post a Comment